<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><?xml-stylesheet href="http://www.blogger.com/styles/atom.css" type="text/css"?><feed xmlns='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' xmlns:georss='http://www.georss.org/georss' xmlns:gd='http://schemas.google.com/g/2005' xmlns:thr='http://purl.org/syndication/thread/1.0'><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709</id><updated>2012-01-02T11:20:42.068-08:00</updated><title type='text'>Ongea na Mike</title><subtitle type='html'></subtitle><link rel='http://schemas.google.com/g/2005#feed' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/posts/default'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default?max-results=100'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/'/><link rel='hub' href='http://pubsubhubbub.appspot.com/'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><generator version='7.00' uri='http://www.blogger.com'>Blogger</generator><openSearch:totalResults>8</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>100</openSearch:itemsPerPage><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-4235440412119191976</id><published>2012-01-01T15:18:00.000-08:00</published><updated>2012-01-02T11:20:42.082-08:00</updated><title type='text'>Buriani Mpendwa John Wilfred Ngahyoma (JW)!</title><content type='html'>Mike Mhagama,Los Angeles-California.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunafunzwa na elimu dunia kutothubutu kumwuuliza mwenyezi mungu maswali ya kwanini,nami kamwe sithobutu kukiuka mwiko huo pamoja na uchungu mkubwa nilionao moyoni kwani Bwana yeye ndiye aliyetoa na yeye pekee ndiye mwenye kutwaa kwa mapenzi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimepokea kwa masikitiko makubwa mno na kwa mshangao kifo cha Kaka yangu,Mjomba,Rafiki na mshauri wangu mkubwa na wa Karibu katika maisha yangu John Wilfred Ngahyoma aliyefariki akiwa katika mapigano na ugonjwa wa kansa ya mapafu uliomsumbua kwa muda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wengi wanaofanya kazi kwenye vyombo vya habari na nje ya hapo wanajua mimi na John ni ndugu wa damu,toka nitoke.Hii ni kutokana na ukaribu niliokuwa nao sio tu kikazi hata binafsi na jinsi alivyokuwa akinitambulisha kwa watu wa nje,nilikuwa karibu sana na Kaka John na tulikuwa pamoja sehemu nyingi na mara kwa mara.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilikaa na John nyumbani kwake kwa miaka zaidi ya 4 mara baada ya kumaliza elimu yangu ya kidato cha nne.Alinitambulishwa kwa kila mtu kuwa mimi ni mdogo wake na alipenda sana watu wafahamu hivyo na si vinginevyo japokuwa yeye ni mtoto wa mwisho kwa Mama yake Bibi Sabina.John alikuwa mkarimu na aliyependa kusaidia kila mtu pale anapoona inafaa.Hakuwa mtu wa maneno maneno wala majungu,John alikuwa tayari kujitoa mhanga ili wengine waepushwe kuingia matatizoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ninaufahamu ukoo wa akina Ngahyoma kwa miongo kadhaa sasa toka utotoni.Sio tu sababu ya ujirani wetu pale Songea lakini pia ndugu zetu pande zote  wanafahamiana na walishiriki pamoja katika masuala mengi ya kijamii na ya kikazi pamoja na hivyo kuwa kama ndugu zaidi ya Ujirani!&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Marehemu Anna Ngahyoma,dada yake Marehemu John Ngahyoma kwa Baba Mkubwa (Askofu Ngahyoma) alikuwa katibu Muhtasi wa Baba yangu mzazi wakati huo Baba yangu akikaimu nafasi ya Ukurugenzi wa Mji pale Songea miaka ya 80 mwishoni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dada Anna alinipenda sana na nilikuwa naye karibu kupita kiasi na ndio ukaribu wangu na ukoo mzima wa Ngahyoma ulianzia hapo.Katika mazungumzo yetu ya kawaida Dada Anna aliwahi kuniuliza siku moja ningependa kuwa nani nikiwa mkubwa? Nilimjibu napenda sana kuwa Mtangazaji kama Alex Shauri (Aliyekuwa Afisa Uhusiano Bima) aliyekuwa akitangaza vipindi vya “Bima Yako”.Alicheka sana na kusema kama napenda kuwa mtangazaji basi inawezekana kwani ana kaka yake anatangaza lakini yeye yuko shirika la NPF ila nitilie mkazo katika kusoma kwani hao watangazaji wamesoma pia.Kaka yake huyo ni John Ngahyoma.Nikakubali na kufuatilia sana vipindi vya John.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baadaye Dada Anna katika maongezi ya kawaida alimhadithia Mama yangu kuhusu navyoweza kunisaidia kufikisha ndoto yangu.Walicheka sana na kuona miye labda ni mtoto na nikikua pengine nitabadili mawazo na kutaka kitu kingine.Dada Anna alinifuatilia kimasomo na alisikitika sana kusikia sikuchaguliwa kwenda shule ya Sekondari ya serikali (sijui kwa nini alidhania hivyo) baada ya kumaliza shule ya msingi lakini nilibahatika kupata nafasi ya kuanza kidato cha kwanza katika shule ya binafsi inayomilikiwa na Umoja wa wazazi mkoani Mbeya iitwayo Chimala Sekondari mwaka 1989.Nilisoma Chimala Sekondari mpaka mwanzoni mwa mwaka 1992 na kuhamia shule nyingine iitwayo Irambo High School mkoani Mbeya ambako nilimaliza kidato cha nne mwaka 1992.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati haya yote yanatokea Mzee wangu alikuwa hayupo tena katika nafasi ile ya Ukurugenzi na alikuwa tayari amerudishwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Ruvuma kama Katibu Tawala na hivyo hakuwa karibu tena na Dada Anna zaidi ya  ujirani wetu.&lt;br /&gt;Pamoja na hayo Dada Anna bado alikuwa akitutembelea na kutembeleana na familia kila nikirudi likizo kutoka shuleni Mbeya na kujua maendeleo yangu kimasomo na kila mara kuniuliza bado unataka kuwa Mtangazaji kama utani nami nilikuwa namuitikia!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilipomaliza kidato cha nne baba yangu alikubali kunisomesha mpaka ngazi ya diploma kuanzia cheti pale TSJ ili nitimize ndoto yangu kwa ushauri wa Dada Anna.Hii ilikuwa mwaka 1992 na msimu wa shule ulikuwa uanze mwaka 1993 mwezi wa tano au saba kama sikosei.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bahati mbaya Baba alifariki mwaka 1993 mwezi March huku akiwa amestaafu utumishi wa umma.Sikubahatika tena kwenda kusoma TSJ kama ilivyopangwa na hivyo kukata tamaa kabisa kuwa mtangazaji kama familia tulivyotaka ili niwe mtangazaji mwenye angalau Diploma kwani mambo ya kifamilia yalikuwa mengi na ukamilifu wa yote hayo ulitaka fedha huku nguzo kuu (Baba Yetu) ikiwa haipo tena nasi! Nilikata tamaa!!!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwaka 1994 John Ngahyoma alikuja Songea kimatembezi na kufikia kwa Dada Anna.Nilitambulishwa kwake na alifurahi sana kusikia napenda kazi aifanyayo.Alinipa misingi na namna gani yeye alisoma na kufikia hapo alipofikia.Alisema kuwa mara nyingi kama una kipaji mashirika mengi yanakusomesha mradi tu uwe na nia na usikate tamaa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John alinishauri nimtafute pindi nikiwa Dar E Salaam ambako nilikuwa nikienda mara kwa mara kutokana na ukoo wa mama yangu kutokea huko.Nilifanya hivyo mwezi uliofuata tu,lakini kwa sababu nilikuwa nikiishi Kimara mbali kidogo ya mji John alishauri ili kuwe na mawasiliano ya karibu na pia kwa sababu nilikuwa karibu sana na mdogo wake John aitwaye Maurice (rafiki yangu wa utotoni),John alinishauri niishi nyumbani kwake Mbagala.John na mdogo wake ni zaidi ya marafiki au majirani na ni zaidi ya ndugu na niliishi nao kwa kuheshimiana kama ndugu wa damu na familia yangu iliridhika kutokana na kujuana kwetu kwa muda mrefu!!Ni vigumu kupata watu wa aina hii siku hizi na dunia yetu hii ya leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilihamia hapo na huku Kaka John akiongea na rafiki zake wa Radio Tanzania kuona kama naweza kufanya mafunzo hapo pia akiangalia uwezekano wa angalau kusoma kiwango cha cheti huko Nyegezi,Mwanza ambako yeye alisoma .Wakati hayo yakiendelea,Mwaka 1995 zilitangazwa nafasi za kazi Radio One ambako John alikuwa akifanya kazi upande wa ITV kama Mhariri wa habari.Alinishauri kutuma maombi na nifanikiwa kuitwa kwenye mahojiano na baadaye kuambiwa kuwa nimeshinda na kupata kazi Radio One!!!!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ilikuwa ni bahati na faraja sana kwangu kwani sio tu niliweza kufanya kile kilichoonekana ndoto mwanzoni na maishani mwangu bali pia kujua kuwa nitalipwa huku nikifanya kazi hiyo tofauti na mwanzo nilipodhani ni mafunzo tu,kitu ambacho sikutarajia hasa nikikumbuka kifo cha mzee wangu na kukosa nafasi ya kujiunga na shule TSJ!Lakini yote ilikuwa mipango ya mungu!!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliishi na John kwa ukaribu sana na alikuwa msiri wangu mkubwa.Mafanikio yangu yalikuwa ya kwake na ya kwake yalikuwa ya kwangu.Nakumbuka nilipata bahati ya kukubalika katika chuo fulani huko Ireland kusomea Diploma ya uandishi wa habari na wakati huo huo kupata nafasi ya kuhudhuria mafunzo US,John ndiye aliyenipa ushauri wa nini cha kufanya kuzingatia umri wangu na huko mbele ingekuwaje kama ningekuwa Ireland au US,Ahsante Kaka John kuwa mkweli na muwazi kwangu na ushauri wako ulikuwa wa busara na ndio ulionifikisha hapa nilipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kutokana na kazi niliyokuwa nikiifanya kuwa na mashabiki,Wengi walitaka kujua niliondoka vipi Tanzania na hata kumfuata John kwa maswali huku wengine wakizusha kuwa nimetoroka bila kuaga kazini,bila kujua kuwa nimeondoka Radio One kwa baraka zote za wakuu wangu na kwa usaidizi mkubwa binafsi wa rafiki yangu Rodney Mutie Mengi (Mungu ailaze pema peponi roho yake).John alibeba mzigo usio wake wa kunijibia maswali kwa watu!!!John alitafsiri makosa ya wengine kama yake na kusaidia kuyatatua bila majigambo!&lt;br /&gt; &lt;br /&gt;Roho ya utu aliyokuwa nayo John ndiyo iliyomfanya wengi wampende situ kwa sababu ya kuonekana kwake kwenye Televisheni kama mmoja ya watangazaji wa awali kabisa nchini au kusikika kwake kwenye chombo cha kimataifa kama BBC bali kutokana na jinsi alivyoishi vyema na watu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John hakunionea haya mimi wala mdogo wake au ndugu yake wa damu pale tulipokosea,alitusema kwa unyenyekevu kama ambavyo angemsema mtu mwingine yeyote mwenye mapungufu ambayo yeye aliyoyaona kwani alisisitiza kuwa aibu yetu ni yake!!! Hakupenda kumbagua mtu na ndio maana mpaka leo nathubutu kusema bila John Ngahyoma na Dada yangu Anna Ngahyoma mimi binafsi nisingeweza kuwepo hapa nilipo kimaisha na kitaaluma,alinitoa kimaso-maso pale nilipokosa muongozo au kukata tamaa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John alikuwa mtu wa kwanza kumtaarifu kuwa nimepata mchumba na alishiriki na kuniwakilisha vyema pamoja na ndugu zangu katika shughuli zote kwa wakwe zangu kama Kaka mkubwa.Pamoja na safari zake za mara kwa mara ndani na nje ya nchi kutokana na majukumu aliyonayo,John alihudhuria vikao vyangu vyote vya harusi kama Kaka Mkubwa wa familia.John hakuwa mnafiki na alikuwa rafiki wa kila mtu!! Muulize Manambi Ismail,Richard Maabadi,Jabir Jabir,Nestor Mapunda,Rukia Mtingwa,Laura George,Betty Mkwassa au Kiyungi Fundikira! Muulize Susan Mungy,Amos Msanjila,Aliko Tshimwela au Bi Asha Mtwangi,Anthery Mushi,Kaka Kaniki au Mzee Masako!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara ya mwisho niliongea na Kaka John kwa matumaini na kwa utani sana akiwa Hospitali India.Nilipata faraja sana!!! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa wanahabari tumempoteza mwenzetu,Upendo,Josephine,Sabina,Casian,Wilfred na Cecy wanamlilia mjomba au "Uncle Fresh" kama tulivozoea kumuita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Edward,Chris,Maurice,Ngalimecha,Julius na wengine wengi ikiwemo mimi binafsi tumempoteza Kaka na mdogo wetu!!!Pole shemeji yangu Faith na watoto,Poleni akina Ngahyoma,Poleni akina Mwingira na ukoo wote! Poleni wanahabari.Mungu atupe nguvu katika wakati huu mgumu! Kaka John kumbukumbu yangu kwako haitofifia milele!Daima nitakukumbuka na wengi kamwe hawatokusahau!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kalale pema mpendwa Kaka John!!!bado tunakulilia,bado hatuamini!! Lakini yote tunamwachia Mungu.Yeye ndiye aliyetoa na yeye ndiye ametwaa.Jina lake litukuzwe. Amen!!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-4235440412119191976?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/4235440412119191976/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=4235440412119191976' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4235440412119191976'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4235440412119191976'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2012/01/buriani-mpendwa-john-wilfred-ngahyoma.html' title='Buriani Mpendwa John Wilfred Ngahyoma (JW)!'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-4029013505709574128</id><published>2009-07-21T14:57:00.000-07:00</published><updated>2009-07-21T16:45:26.507-07:00</updated><title type='text'>USHAURI WA BURE KWA WANAMUZIKI WA KIZAZI KIPYA TANZANIA.</title><content type='html'>                                                               Na Mike Mhagama,Los Angeles.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;Kuna matukio kadhaa muhimu ambayo tumepata kuyasikia kutoka kwenye vyombo vya habari kuhusu wanamuziki na muziki wa kizazi kipya.Ni vyema kuwasikia wanamuziki wetu wakitangazwa lakini ingekuwa vyema zaidi kama habari hizo zingekuwa ni zile zenye mtazamo wa kuigwa na sio wa iga ufe.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kutoka Usagara mpaka Njombe,kutoka Dar mpaka Mwanza wanamuziki wetu sasa hivi sasa wamefanya kutamba kwa habari zao "chafu chafu" magazetini ni dili  au fasheni fulani.Cha kusikitisha zaidi wengi wa wanayoipa aina hii ya muziki jina chafu  ni wale wenye "&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;singo&lt;/span&gt;" tu na si wanamuziki nguli waliotoa albamu kadhaa zikasikika na kufanya vyema ndani na nje ya Tanzania.Ni ukweli tusiokataa pia kuwa wapo baadhi ya magubeli katika kueneza uchafu huu wa matukio mabaya mabaya ndio maana kwa ujumla nikaona ni vyema kama mpenzi nambari wani wa muziki huu nikawapa ushauri wa bure bwelele.Atayesikia na asikie na asiyetaka basi lwake na aweke pamba masikioni kabla ya kumfika litakalomfika!&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Mwanamuziki nguli katika miondoko ya dansi nchini Tanzania na ninayemheshimu sana Maalim Ngurumo alikaririwa hivi karibuni akisema wanamuziki wa kizazi kipya ni kama pipi aina ya"&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;bazoka&lt;/span&gt;" na wengi wao wanakaribia kuisha utamu kwani wananoga mara moja tu halafu basi.Ngurumo hakuyasema maneno haya kwa mzaha kwani ni mtu anayeheshimika kimuziki na hata kiumri na kwa hivyo maneno yake lazima yachuliwe kwa uzito unaostahili na sio juu juu tu.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Maneno haya mazito aliyoyanena Mzee Ngurumo kutokana na baadhi ya tabia za wanamuziki wenyewe yaliwachefua vilivyo  baadhi ya wanamuziki wakongwe katika muziki wa kizazi kipya,kati yao ni Prof Jay na AY ambao walipinga kauli hiyo kwa kusema sio ya kuwatakia mema lakini walishindwa kumpinga moja kwa moja Ngurumo kwani waliona ukweli ndani ya maneno yake na kuongezea kusema ni kweli baadhi ya wanamuziki wachache ni lazima wajiandae kwanza kabla ya kufikiria kuingia kwenye fani kwa kukurupuka na kutoa "&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Singo&lt;/span&gt;" halafu kuchafua hali ya hewa na kesho yake hawasikiki tena.Kwani kwa wao kufanya hivyo ndipo kunapompa fursa mkongwe kama Maalimu kuthibitisha kauli yake na kuufanya muziki mzima wa kizazi kipya kuonekana kama pipi ya bazoka bila kujali nani ni nani kwani falsafa inasema samaki mooja akioza basi kapu lote litatoa harufu ya uvundo.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Maneno ya wanamuziki hawa wa pande hizi mbili yana maana na mwelekeo sawia kimtazamo.Wanamuziki hawa si kwamba wanauchukia muziki huu na chipukizi wake au labda wana wivu kwa vipaji vipya vinavoibuka kila kukicha la hasha! wamefanya hivi kutokana na mapenzi yao ya dhati kwa muziki huu ambapo kama wao nami pia sitokubali wachache waupe jina baya kwani nguvu nyingi na za watu wengi zimetumika kuufikisha hapa ulipo.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Ninayoyanena hapa kamwe hayamlengi mtu mmoja mmoja bali jamii nzima ya wana &lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Bongo Flava&lt;/span&gt;.Ni changamoto kwa wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya kuona kwamba wasipoangalia na kutafakari kwa kina maneno ya akina Maalim Ngurumo basi si wanamuziki wapya tu wanaotoka watakaochungulia kaburi na kuzimika kabisa katika fani bali hata muziki wenyewe utakuwa kwenye wakati mgumu sana na hakuna atakayethubutu  kuurejesha katika anga kuu pindi utakapotoweka.Hii ni kuwashauri tu wanamuziki wa kizazi kipya ya kuwa wasipokuwa waangalifu matunda ya kazi zao na juhudi zote za wakongwe waliopigania muziki huu  kufa na kupona,kwa kukubalina kupokea kwao kashfa na matusi zitakuwa ni kazi bure na kwamba mapinduzi yaliyokuja na muziki huu kuzikwa kabisa kwa staili ya kifo cha mende,miguu juu.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;labda kwa kusoma haya kuna mtakaoguna..well,ni haki yenu na naomba mjue sina hasira bali ni uchungu kwa wadogo zangu wenye tabia hizi chafu za kuwafanya kujichora magazetini kila kukicha.Najuta kusema kuwa ulimbukeni wao unaonesha dira na pengine ni ishara tosha kwa wasikilizaji wenu na hata wakongwe kama Ngurumo kuthubutu kusema kuwa muziki huu sasa unakosa mwelekeo.Ni nyinyi  wanamuziki wenyewe mnaoupa majaribu yasiyo na msingi bila kujali kuwa muziki huu ukififia basi na nyie hamna ajira.Wanamuziki wetu lazima mtambue kuwa kama mtaendelea na ubabaishaji na tabia zenu chafu za kutaka umaarufu wa haraka haraka huku mkiupa jina baya na kuufanya muziki huu uanze kudharaulika basi muwe tayari kubeba lawama na kuhukumiwa kwa matendo yanayopeleka ukomo wa fani hii.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kwa nini kila siku tusikie au kusoma juu yenu tu? ati mwanamuziki fulani wa kizazi kipya kafumaniwa na mke wa mtu au kapiga picha za uchi? mbona kuna wenzenu wa filamu,wachezaji wa mpira wa miguu nk? kwanini wasiwe wao kila kukicha na habari hizo chafu magazetini? halafu tunajiuliza kwa nini udhamini mkubwa unaenda kwenye soka badala ya muziki? kwa sababu wanaohusika na soka ni watu wanaojiheshimu na wenye heshima zao japo sio wote lakini angalau walio wengi.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kupigana hadharani,kuchomana visu,kunyan'ganyana wanawake,kugombania mabinti,ulevi wa kupindukia,ubabe kwa watu wasio na majina,ulimbukeni/majigambo yasio na kichwa wala miguu kwenye sehemu za starehe kama baa n.k ni baadhi tu ya yale ninayoyakemea hapa na ni yale ambayo yamekuwa yakihusihwa kwa kiasi kikubwa (80%)na wanamuziki wetu wa kizazi kipya huko nyumbani Tanzania.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kama nilivyosema hapo juu haya mambo pengine yapo kwenye fani zingine na si kwa &lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Bongo Flava&lt;/span&gt; peke yake.Kinachokera ni kuona nyie ndio mnaoongoza kwenye uchafu huu.Nashindwa kukubali kuona kile ambacho  sote tulikipigania kwa nguvu zote kikikaribia kuchungulia kaburi na kupakwa matope na wahuni wachache.Muziki huu wa kizazi kipya  na wanamuziki wake lazima wawe zaidi ya mashairi jukwaani na nje ya jukwaa.Ni lazima wakubali kuwa sehemu ya maisha ndani ya jamii tunayoilenga na muziki wetu,jamii hii ndio inayotupa kula na ndio waajiri wetu wakuu na lazima tuipe heshima inayostahili.Ni vyema kuweka mikakati ya kudhibiti hali hii mapema ili muziki huu urudi katika malengo yake ya awali chini ya mwelekeo thabiti  na sio ubabaishaji.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Nimepata faraja sana kusikia hivi karibuni kumeanzishwa umoja wa wanamuziki huu wakiongoza na Judith "Manka" Wambura au lady Jay Dee na Banana Zahor.Hawa ni watu makini si tu wawapo jukwaani lakini hata wanapokuwa nje ya jukwaa  "&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;uraiani&lt;/span&gt;'.Kuchaguliwa kwao kuwaongoza wenzao kuwe ni changamoto kwao na waweze kuwashawishi wenzao kuwa mfano wa kuigwa na si mfano wa kubezwa kama ilivyo sasa ambapo kila gazeti lazima liwe na stori mbaya ya mwana &lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Bongo&lt;/span&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt; Flava&lt;/span&gt;.Inatia kinyaa kusikia wanamuziki wengine eti wanauza stori chafu kama hizi kwa magazeti ya udaku ili kupata "&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Publicity&lt;/span&gt;"...that's cheap na inatia aibu.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Bongo Flava Unity isikubali kuruhusu wahuni wachache waitangaze vibaya fani yao.Kamwe wasikubali jasho lao au la wenzao liende bure hasa kwa dosari za watu wachache wenye kiburi kisichokuwa na maana.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Ulevi wa kupindukia,iwe pombe/bangi  au ngono zembe sio sifa ambayo mwana &lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Bongo Flava&lt;/span&gt; anatakiwa kuwa nayo ili awe juu bali ni sifa ambayo mtu yoyote hayawani asiyeheshimu juhudi za wenzie na mwenye laana anatakiwa kuvikwa.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kuna mengi ya kurekebishika ambayo ningeweza kuyaandika hapa,lakini kwa ujumla wake hayo niliyoaandika hapo juu yanatoa mwanga na mshtuko kwenu kama wadogo zangu kuwa wakati sasa umefika wa kuuchukulia muziki huu kama ajira inayowaweka wengi wenu mjini hapo na si vinginevyo.Hakika tusipoangalia muziki wa kizazi kipya na wanamuziki wake tunaoushimu na kuupenda sana,si punde unaweza kuwa hadithi ya utamu wa "&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;bazoka&lt;/span&gt;" na sijui tutamlaumu nani....&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Alamsiki..&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-4029013505709574128?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/4029013505709574128/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=4029013505709574128' title='3 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4029013505709574128'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4029013505709574128'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2009/07/ushauri-wa-bure-kwa-wanamuziki-wa.html' title='USHAURI WA BURE KWA WANAMUZIKI WA KIZAZI KIPYA TANZANIA.'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>3</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-4903295105942107549</id><published>2008-09-13T11:19:00.000-07:00</published><updated>2008-09-13T11:21:43.789-07:00</updated><title type='text'></title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://3.bp.blogspot.com/_unbAPpKBNZ4/SMwEpzotDUI/AAAAAAAAAB8/BhKKBSnX_o0/s1600-h/013_13.JPG"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://3.bp.blogspot.com/_unbAPpKBNZ4/SMwEpzotDUI/AAAAAAAAAB8/BhKKBSnX_o0/s320/013_13.JPG" border="0" alt="" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5245572782261865794" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;Millenia mwaka 2000 nikiwa na wanamuziki wakongwe Fadhili Nkurlu na Inno Mfalingundi Galinoma,Minneapolis. &lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-4903295105942107549?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/4903295105942107549/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=4903295105942107549' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4903295105942107549'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4903295105942107549'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2008/09/millenia-mwaka-2000-nikiwa-na.html' title=''/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://3.bp.blogspot.com/_unbAPpKBNZ4/SMwEpzotDUI/AAAAAAAAAB8/BhKKBSnX_o0/s72-c/013_13.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-1676500360594273003</id><published>2008-07-03T18:53:00.001-07:00</published><updated>2008-07-06T15:44:32.038-07:00</updated><title type='text'>SEHEMU YA MWISHO</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://bp2.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SG2ELihhIoI/AAAAAAAAABY/2_VyT4H3dA4/s1600-h/DSC00467.JPG"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://bp2.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SG2ELihhIoI/AAAAAAAAABY/2_VyT4H3dA4/s320/DSC00467.JPG" border="0" alt="" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5218972876973089410" /&gt;&lt;/a&gt;(&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Pichani: Mimi, Dj Runkim "Zipompapompa" Ramadhani na Dj Sebastian Maganga, Dar-Tanzania&lt;/span&gt;) &lt;br /&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-weight: bold;"&gt;K&lt;/span&gt;ufikia hatua hii basi labda niseme tu kuwa imefika wakati wanamuziki wa Hip Hop na Bongo Flava leo hii wana nafasi yao katika jamii ya Tanzania na wanapaswa kuenziwa,kukumbukwa na kuheshimika bila kuchanganya aina hizi mbili za muziki kwani ni vitu viwili tofauti kabisa lakini lengo likiwa moja.Kuna mambo mawili ambayo nadhani yakifanyika basi angalau kumbukumbu ya wale wakongwe walioanzisha harakati na mapinduzi katika muziki huu watadumishwa na wale wapya watajifunza kutokana na kuwaenzi wakongwe hawa.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Hapa tusisahau pia wakongwe waliokuwa wakipiga ianyoitwa Hard Core HipHop kama Fresh XE ambaye sidhani kama alibahatika kurekodi,Samia X,GWM,E-Attack,Underground Soul,Hasheem,KU Crew,Nigga One,D-Rob au II Proud na wengineo ambao walikuwapo hata kabla ya kipindi cha DJ SHOW au Radio One kuanza lakini hawakuwa na sehemu ya kuutangaza muziki wao.Hawa kamwe hawatasahaulika na wana heshima kubwa sana kwenye muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Bila kutegemea "Awards" ambazo zinaonekana kuwa na dosari kila zinapofanyika kila mwaka kwa tuhuma za upendeleo nadhani imefika wakati mwafaka kwa muziki huu na wanamuziki wake kuwa na tuzo zake maalum zitakazofanyika kila mwaka na kuzitofautisha kabisa na zile tulizozioea za muziki mchanganyiko.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kuwepo na utaratibu wa kujumuisha wiki ya tuzo hizo na usaidiaji wa jamii kwa wakongwe watakotumikiwa tuzo hizo kutembelea baadhi ya shule za msingi au sekondari na kutoa changamoto ya maisha na elimu juu ya muziki huu kwa ujumla kwa kizazi hiki kijacho.Pia hata kushiriki nao katika shughuli za usafi wa mazingira kwa siku hiyo.Huu ni mchango tosha na ishara kuwa muziki huu si uhuni ni sehemu ya maisha kwa kizazi kipya.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Vile vile sehemu ya mapato na udhamini wa onesho hili iende kusaidia shule masikini au ya watoto wasiobahatika na wenye ulemavu wa namna moja au nyingine.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kwa kufanya haya na mengineyo mengi muziki huu sio tu utakuwa ni wenye kujijengea heshima bali kuweka kumbukumbu kubwa ya mapinduzi kwenye ulimwengu wa muziki Tanzania na hadhi yake kuwa ni ile isiyofutika kwa urahisi machoni na akilini mwa kizazi cha sasa na hata kile kijacho kwa muda mrefu.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt; &lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-1676500360594273003?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/1676500360594273003/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=1676500360594273003' title='2 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/1676500360594273003'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/1676500360594273003'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2008/07/sehemu-ya-mwisho.html' title='SEHEMU YA MWISHO'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://bp2.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SG2ELihhIoI/AAAAAAAAABY/2_VyT4H3dA4/s72-c/DSC00467.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>2</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-7582057049227675079</id><published>2008-06-21T14:45:00.000-07:00</published><updated>2008-07-06T15:33:06.799-07:00</updated><title type='text'>SEHEMU TA TATU</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://bp0.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SF13ZkRPlBI/AAAAAAAAAA4/sl01O3AV4wY/s1600-h/006_6.JPG"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://bp0.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SF13ZkRPlBI/AAAAAAAAAA4/sl01O3AV4wY/s320/006_6.JPG" border="0" alt="" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5214455224681337874" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;(&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Pichani nikiwa na mwanzilishi wa mtandao wa africanhiphop.com na Madunia Foundation Dj Thomas "J4" Gesthuzen tukijadili jambo juu ya ukuzaji wa muziki huu kwa njia ya internet huko Holland,hii ilikuwa mwaka 1997&lt;/span&gt;).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-weight: bold;"&gt;                                                                              SEHEMU YA III&lt;/span&gt;.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;div&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-weight: bold;"&gt;K&lt;/span&gt;wa vile kwa namna moja au nyingine harakati zilionekana kuanza kuzaa matunda,nami niliona ni vyema nikauchukua mwanya huu kuzaa kile ambacho mwenzangu Master T alikuwa mstari wa mbele kukingia kifua ili kufanikisha azma ya kuwaweka vijana wa Tanzania na muziki wao wa kizazi kipya mbele ya watanzania lakini huku kukiwa na msisitizo wa "cha kwetu".&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilibahatika kufanya mazungumzo na mmoja wa wana Hip Hop mahiri nchini anayetokea kwenye kundi la Kwanza Unit Kibacha "KBC"  Singo ambaye tulikuwa tukifahamiana kwa muda mrefu toka mkoani Mbeya ambako sote tulikuwa tukisoma miaka ya mwanzoni ya tisini.KBC alikuwa ni msomaji mzuri na muelewa wa mambo mengi ya Hip Hop.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nilimweleza azma yangu ya kujaribu kuuingiza muziki huu hewani lakini kwa ushauri wa nini kifanyike ili tusichekwe kwa kuonekana tunaiga sana umarekani.KBC alicheka lakini alikubaliana nami na kusema hatuwezi kuibadilisha Hip Hop kufuata midundo yetu lakini tunaweza kuibadilisha kulingana na lugha pia vionjo vya kwetu.Lakini kwanza KBC alisema si kila mtu anaweza kufanya Hip Hop na lazima anayetaka kuingia katika game lazima ajue misingi ya muziki wenyewe.Nilikubali maoni ya KBC na niliuomba uongozi wa Radio one kugawa saa nzima,kuanzia saa 12 mpaka saa moja jioni katika siku moja ya wiki ili kutimiza haja hiyo,hasa hasa kuutenga muda huo kwa muziki wa Rap/Hip Hop tu na si kitu kingine ili kuupa muziki huu nafasi zaidi ya kusikika na kutambulika tofauti kabisa na ule wa kutoka The Bronx,Dirty Dirty South au South Central L.A.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Niliomba kwa uongozi ili KBC aongoze kipindi hicho lakini uongozi kwa sababu za kueleweka ulikataa na kunitaka niendeshe kipindi hicho mimi mwenyewe na KBC awe mgeni maalumu au mtoa mada katika kipindi hicho wakati wowote akiwa na nafasi.Kipindi kilikwenda hewani kwa mara ya kwanza na KBC alikuwa &lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;regular&lt;span class="Apple-style-span" style="font-weight: bold;"&gt;.&lt;/span&gt;&lt;/span&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;&lt;br /&gt;&lt;/span&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Matokeo yalikuwa mazuri kwani vijana wengi walikipokea kwa mikono  miwili na kushukuru mchango wa KBC katika kipindi hiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hip Hop ya Tanzania ilianza kubadilika na kuanza kuwa na sura na mwelekeo wa Tanzania kama tulivyotarajia kwani kwa mara ya kwanza mkali mwingine wa Hip Hop Ramadhani "Chief Rhymson" Mponjika alitoa single yake kwa kumshirikisha mkongwe wa miondoko ya dansi aitwaye Hassan Seyvunde na kibao ambacho kilitamba sana sio kwenye Radio tu hata kwenye TV kutokana na maudhui yake.Pia kundi lao la Kwanza Unit walikubali mwito na kuibuka na kibao kiitwacho &lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Msafiri&lt;/span&gt; ambapo rekodi ilikuwa na kiitikio kilichodurufu rekodi ya mkongwe wa muziki wa dansi Tanzania al maarufu kama Mzee Mzima King Kikii Mwanza Mpango.King Kikii naye alijumuika na familia ya Kwanza Unit katika matamasha mbali mbali kuwapiga tafu na mara wimbo huo ulipopigwa katika matamasha hayo mapokeo yalikuwa ni ya kuridhisha na huo ndio ukawa mwanzo wa Hip Hop ya Tanzania kupanda chati na kukubalika zaidi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati haya yote yanatokea mkongwe mwingine kwa jina la 2Proud (sasa Sugu) naye hakuwa nyuma alitoa nyimbo ambazo zilikuwa gumzo na zenye ujumbe wa moja kwa moja kwa viongozi wa siasa Tanzania mpaka aliyekuwa Mratibu wa vipindi wa Radio One Charles Hillary alianza kukubali kazi za wasanii wa kizazi kipya na kuamua kuvunja baadhi ya masharti ambayo hapo mwanzo yalikuwa ni kikwazo.Charles Hillary kwa mara ya kwanza alikubali kupiga wimbo wa msanii wa huyu IIProud uitwao "&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Ni Mimi"&lt;/span&gt; katika moja ya vipindi ambavyo alikuwa akiviendesha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ulikuwa ni mwanzo mzuri na upanuzi mkubwa kwa muziki wa Hip Hop Tanzania ambao sasa ulianza kushamiri kila kona na kwa kasi kubwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini changamoto haikuwa kwenye Hip Hop ya Tanzania tu bali hata muziki wa dansi nao ulianza kubadilika kutokana na wakati.Kama ilivyo kwa KBC na mchanganuo wake wa mawazo kwenye kipindi changu cha Rap time ambacho sio siri kiliwafungua macho vijana wengi waliotaka kuingia katika muizki katika miaka ya 90 ukiachilia wale wakongwe,basi katika dansi nako kulikuwa na mapinduzi yake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sote tunakumbuka bendi kama Diamond Sound ambayo ilikuwa ikipiga nyimbo nyingi za Congo na zikiimbwa kwa lugha ya kilingala.Niliwahi kumwalika kiongozi wa band hiyo Elliston Angai katika kipindi cha DJ Show na rapa wake mashuhuri Allan Mulumba Nkashama na kufanya nao mazungumzo ni namna gani wanaweza kushirikisha vionjo vya Tanzania zaidi katika nyimbo zao na Rap zao.Bila kusita walikaribisha wazo hilo na kama ilikuwa ni mgongano wa mawazo kumbe nao walikuwa wanatafakari namna ya kutawala soko la muziki wao kwa kuuza CD ambazo muziki wake utakuwa na mtazamo na ladha ya Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Allain Mulumba kutokana na ubunifu wake alikuja na rap yake ya kwanza kabisa baada ya changamoto hiyo kwenye DJ Show ambayo alitumia tangazo la sabuni kuonesha muonjo huo.Tangazo lile lilikuwa na maneno kama "&lt;span style="font-style:italic;"&gt;Omari mbona unajikuna sana,sio siri mamaa! ninawashwa sana ngwarariii ngwararaaa"&lt;/span&gt;.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndipo sote tulipokubali maapokezi ya muziki na kwa kutumia lugha yetu kumbe unalipa.Ukumbi wa Silent Inn ulilipuka kwa furaha ya Rap hiyo ambayo kwa mara ya kwanza ilipigwa usiku huo na kutambulishwa rasmi,mashuhuda wenzangu katika mapinduzi haya usiku huo pale Silent Inn walikuwa waandishi wenzangu Sebastian Maganga (Radio One),Farouq Karim (ITV Zanzibar),John Ngahyoma (ITV Dar) na Chacha Maginga (sasa TBC1) .Baada ya hapo tulishuhudia band nyingi zikiiga sana mtindo huu na kuibuka na rap za kiswahili kwenye miziki waliyokuwa wakipiga ambayo ina asili ya Congo.Tunakumbuka bendi kama FM Musica na zingine ambazo zilifuata nyayo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nanyambulisha haya kwa makusudi ili kuweka kumbukumbu sawa na kwa vile kuna   kusahahulika kwa matukio muhimu kama haya hasa inapofika wakati wa watu aidha wasiojua kumbukumbu hizi au kwa makusudi ya kukidhiana wanaandika zinazoitwa historia juu ya mabadiliko ya muziki wa kizazi kipya Tanzania bila ya kutaja mambo muhimu kama haya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na nikiri wazi kuwa pamoja na kuwepo kwa kipindi cha DJ Show ambacho ni cha kwanza kutambulisha muziki huu wa kizazi kipya hewani na kuwa kipindi pekee chenye heshima hiyo kabla ya kingine chochote,hivi leo husikii wengi wakikipa heshima yake na pengine kukisahau kabisa katika kumbukumbu za muziki huu tunaousheherekea hivi leo.Waulize wanamuziki wakongwe katika anga za muziki huu watakwambia ukweli huu.Pia kumekuwa na kusahaulika kwa waandishi wa kwanza kabisa kuandika habari za wanamuziki hawa kwenye makala na hata kuwafanyia mahojiano kwa mara ya kwanza.Waandishi kama Angetileh Osiah,Tom Kirumbi,Albert Memba ,Ibra Poza,Issa Michuzi au Juma Pinto. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukirudi kwenye Radio lazima nikubali baadaye pia kulikuwa na upinzani na vituo vingine ambavyo navyo viliendeleza muziki huu wa kizazi kipya kwa kasi kubwa sana.Pia watayarishaji wa muziki kama Enrique "Rick" Figueredo wa Sound Crafters pale Temeke,Joakim "Master Jay" Kimario wa MMJ Production,Boniphas "Bonny Luv" Kilosa wa Mawingu Studios,Paul "P" Funk wa Bongo Records (alianzisha kundi la vijna wa miaka saba lililopiga HipHop),Marlon Linje wa Don Bosco studio.Shukurani kwa kipindi cha Dr Beat chini ya KBC na Dj Bonny "Luv" Kilosa na Othman "OJ" Njaidi ambao waliendeleza libeneke katika mtindo ule ule wa ushindani lakini tukiwa marafiki wa karibu na kubadilishana mawazo mara kwa mara kwani sote lengo letu lilikuwa moja.Dr Beat ilikuwa chini ya Clouds FM.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia wadhamini na mapromota ambao walikuwa na moyo wa dhati katika kuendeleza sana hii ya muziki wa kizazi kipya.Na upozungumzia muziki huu basi huwezi kumsahahu Joseph 'Joe" Kussaga na Abdulhakim Magomelo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mimi binafsi mbali ya mkongwe Taji Liundi ambaye alifungua njia ya mapambano na harakati ili kuupa muziki huu nafasi yake kama ilivyo dansi na aina nyengine ya muziki,kamwe sitomsahahukijana mwenye akili "Genius" Dj Sebastian Maganga ambaye alipokea kwa dhati mikoba ya DJ SHOW baada ya miye kuachia ngazi.Sebastian ana nafasi ya pekee sana katika muziki huu tangu alipojiunga na Radio One toka Radio Tumaini,ikumbukwe pia Sebastian ni mwana HipHop aliyetoka na kundi la Afro Reign toka miaka hiyoo.Sebastian ni mbunifu na ndio yeye aliyenisukuma zaidi katika kuibadili DJ Show moja kwa moja na kuachana na nyimbo nyingi za Marekani katika kipindi cha DJ SHOW na pole pole tuliweza kufanikiwa kwa kushirikiana na DJ Jumanne kutoka Holland ambaye alitutengenezea promo nyingi za kipindi na kubadili usikivu wa kipindi hiki kutoka muziki wa Snoopy Dogg/Dr Dre mpaka ule wa akina Mr II/Kwanza Unit.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na katika kufanikisha hilo kwa vile DJ Show ilikuwa inapiga muziki mchanganyiko lakini wa kileo.Siku moja tukiwa kwenye kipindi Sebastian aligusia mfumo wa kutenga muziki katika dakika 30 kila genre,kama tunapiga Reggae basi alishauri iwe dakika 30,kama R&amp;amp;B ya Tanzania basi tutenge dakika 30 nk.Nilikubaliana na wazo hilo kwani lingetufanya tutoe nafasi sawa kwa kila aina ya mtindo na sio upendeleo wa kupiga Hip Hop au R&amp;amp;B tu masaa yote mawili ya kipindi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ilipofika dakika 30 za muziki wa R &amp;amp; B,siku hiyo nilikuwa kwenye usukani na kwa mbwembwe nilicheza nyimbo ya kundi la R&amp;amp;B lililoitwa 4Krewz Flava na baadaye kuiunganisha na nyimbo nyingine ya Unique Sistaz.Kwa vile midundo,mpangilio,lugha na utaalamu wa muziki wenyewe kamwe huwezi kuufananisha na ule wa Soul 4 Real au SWV kutoka Marekani,tulipenda tutofautishe kidogo kati ya aina hizi mbili na ndipo session hii niliibatiza jina ambalo lingetofautisha R&amp;amp;B ya Marekani na ile ya kwetu....niliipa session hii jina la BONGO FLAVA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hii ilikuwa mwaka 1996 na ndio ulikuwa mwanzo wa neno BONGO FLAVA likiwa na maana muziki wenye mahadhi ya nje lakini wenye vionjo na ladha ya Tanzania na si vinginevyo lengo kuu ni kuitofautisha na muziki ule wa Marekani.Hip Hop ya Tanzania ilibaki na itabaki vile vile kama ilivyo,ila muziki wowote ule wa nje,mbali ya Hip Hop na DANSI ya Tanzania niliuita na kuufahamishakwa umma wa watanzania kama BONGO FLAVA ndani ya kipindi cha DJ SHOW cha Radio One.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nikifikia tamati ya mtazamo wangu na jinsi nilivyoshuhudia muziki huu ukikua pengine kumekuwa na ubishi ambao kwa maana halisi nimeonelea nao niudodose kidogo hii leo.Nilipokuwa nyumbani Tanzania nilipata bahati ya kutembelea Clouds FM ambako mwenzangu Sebastian Maganga sasa ni Mkuu wa Vipindi na aligusia suala hili la chimbuko zima la muziki huu na neno BONGO FLAVA.Niliweka haya unayoyasoma wewe hapa bloguni kama yalivyo na niliomba yeyote mwenye kuona tofauti na ninauona ukweli kujitokeza lakini hakutokea mtu kupinga.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Nasema hivi kwa vile huko nyuma kuna waliodiriki kujitokeza/kujitangaza hapo mwanzo na kudai kuwa neno hili BONGO FLAVA ni jina lililotokana au kutungwa na wao,kitu ambacho mimi na mwenzangu Sebastian Maganga tunakipinga kwa sababu tunajua ukweli uko wapi.Watu hawa (tunafahamiana fika) waliombwa kuja studio za Clouds FM siku hiyo katika mahojiano maalum na kuuthibitishia umma juu ya dai lao lakini hakuna aliyetokea.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli kila mtu na mtazamo wake katika kila jambo kutokana na alivyolishuhudia lakini ni vyema tukawa wakweli kidogo bila kupindisha mambo pale tunapotaka kuuhabarisha umma juu ya yale tunayotaka wayafahamu.Katika mnyambulisho huu hapa juu sio lengo wala nia yangu kumsuta mtu na inawezekana kabisa kama binadamu wa kawaida kuna mambo nimeyasahau,kama ndivyo basi ni vyema tukasahihishana ili kurekebisha mambo na sio kudanganya kwa kudhani ukweli kamwe hautojulikana na ndio maana nimeamua kuandika haya ili kuweka yale ninayoyajua wazi kwa faida ya kizazi kijacho na hata cha sasa ambacho kimekuwa kikipotoshwa na wachache.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Na kwa kufanya hivi sina nia hata kidogo ya kutaka au kuuukwa umaarufu,kwani nimekuwa maarufu toka nina miaka 19 na sihitaji wala silazimishi kuwa maarufu hivi leo. &lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Ieleweke kuwa haya yote ni katika kutoa elimu kama shuhuda wa mapinduzi ya muziki huu Tanzania kwani kumekuwa dhahiri na upotoshaji wa makusudi au wa kutojijua inapokuja katika mambo muhimu yanaohusu muziki wa kizazi kipya Tanzania.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Kwa mfano neno hili la BONGO FLAVA lilizaliwa na kutokea katika kipindi cha DJ Show na si vinginevyo kama ambavyo imekuwa ikidaiwa katika zinazoitwa historia za muziki huu wa kizazi kipya kutoka vianzio mbali mbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mfano mwingine hai ni ule kuwa kuna kuna wanaosema TANZANIA MUSIC AWARDS imeanzishwa na mwanamuziki James Dandu (ambaye alikuwa ni rafiki yangu mkubwa) lakini watu wanasahau kuwa TANZANIA MUSIC AWARDS ilianzishwa na mwanamuziki wa zamani wa bendi ya Mawenzi/Prodyuza John Kagaruki chini ya kampuni yake ya Serengeti Production kwa kushirikiana na BASATA mwaka 1997 na sherehe za kwanza kabisa ambazo zilirushwa live na kituo cha ITV zilifanyika pale Whitesand Hotel.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni kweli mwaka uliofuata sherehe hizi hazikufanyika tena na zilipwaya.Lakini tusisahau kuwa mwaka 2000 kampuni ya Look Promotion kwa kushirikiana na Clouds FM walifanya tena onesho hili ikiwa ni mara ya pili kufanyika Tanzania.Na mwaka uliofuata bia ya Kilimanjaro kwa kushirikiana na mwanamuziki James "CJ MASSIVE" Dandu na kampuni yake ya Dandu Planet walizindua upya sherehe hizi ambazo zimekuwa zikifanyika kila mwaka toka wakati huo.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;Mifano kama hii na mingineyo mingi tu inaleta mushkeri hasa inavyopotoshwa kwa makusudi ilhali mashuhuda wake tupo tena tukiwa hai.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Inaendelea juu..&lt;/span&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-7582057049227675079?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/7582057049227675079/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=7582057049227675079' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/7582057049227675079'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/7582057049227675079'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2008/06/bongo-flava-na-uhalisi-wake.html' title='SEHEMU TA TATU'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://bp0.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SF13ZkRPlBI/AAAAAAAAAA4/sl01O3AV4wY/s72-c/006_6.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-4283190478852580713</id><published>2008-06-12T19:24:00.000-07:00</published><updated>2008-07-03T19:16:18.915-07:00</updated><title type='text'>SEHEMU YA PILI.</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://bp1.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SFHhS3LP1DI/AAAAAAAAAAo/58rktFddAR8/s1600-h/sc005a1d8a.jpg"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://bp1.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SFHhS3LP1DI/AAAAAAAAAAo/58rktFddAR8/s320/sc005a1d8a.jpg" border="0" alt="" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5211193958009394226" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;(Hili ni kava la albamu  mojawapo na za mwanzo kabisa kutolewa na mwanamuziki wa kizazi kipya Tanzania Ibony Moalim,Albamu inaitwa Never Gonna Change Feelin')&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;                                                                       &lt;div&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-weight: bold;"&gt;SEHEMU YA II.&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 1994 kituo cha Radio kilikuwa kimoja tu kinachomilikiwa na serikali na wanamuziki wengi wa awali Tanzania walitambulika kutokana na nyimbo zao kupigwa katika kituo hicho hasa kwenye vipindi mbali mbali hasa kipindi maarufu cha kilabu Raha Leo Show.Japokuwa hakukuwa na mfumo maalumu wa mahojiano na wanamuziki ndani ya Radio Tanzania lakini kipindi hiki kilionekana kumaliza karibu kila kitu katika utambulishi wao jkwaani na mpaka jina la mpiga ala au sauti wanazoimba kutoka safu ya mbele,kati hata nyuma.Mara nyingi onesho hili lilikuwa likifanyika LIVE.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wanamuziki ninaowazungumzia ambao walipewa nafasi kwenye kipindi kama hiki ni wale waliokuwa wakipiga muziki wa dansi na pengine taarabu na kwaya japo hawa hawakuwa na nafasi sana wakati huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mara baada ya serikali kulegeza masharti kidogo kwenye soko huria,hatimaye watu binafsi waliruhusiwa kuanzisha Radio binafsi na kwa kuanzia walipewa masafa mafupi kwanza kwa sababu za kiusalama na kupima uwezo wa kumiliki na kuendesha chombo hiki muhimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Moja kati ya Radio hizo za mwanzo kuanzishwa ni Radio One Stereo iliyokuwa ikipatikana katika Megahartz 99.6 FM na kuanzishwa kwa kituo hiki ama kwa hakika ilikuwa ni mwisho wa ukiritimba na ushindani ulianza rasmi.Baadhi ya watangazaji waanzilishi ambao waliombwa na mmiliki ambaye ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Mzee Reginald Abraham Mengi ni Mikidadi Mahamoud ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Utangazaji,Charles Hillary aliyekuwa Mtayarishaji Mkuu wa vipindi na baadaye Mratibu wa kituo na Julius Nyaisangah aliyesimamia vipindi vya burudani na usomaji habari.Hawa wote walitokea Radio Tanzania Dar Es salaam.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mchango wao kwa watangazaji chipukizi ni mkubwa na haupimiki kwa wale ambao walipitia mikononi mwa hawa wakongwe bila shaka watakubaliana nami.Walihimiza kufanya kazi kitaaluma ,walitoa mafunzo na nidhamu ya hali ya juu tuwapo kazini juu ya utangazaji.Hakika walifunguaa ukurasa mpya kwenye kitabu cha utangazaji Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Darasa la kwanza kuajiriwa mwaka 1994 lilikuwa na chipukizi kama Taji "Master T" Liundi,Deo "Best Friend" Mshigeni,Flora Nducha na Runkim Ramadhani Nyamka.Kila mtu alipewa angle/nafasi yake ya kujidai na kipindi anachoweza kumudu.Mfano Taji Liundi alikuwa katika vipindi vya muziki vyenye kutoa maudhui na elimu juu ya mitindo mbali mbali ya muziki na fashion,Taji alikuwa ni mchambuzi.Runkim "Zipompapompa" Nyamka yeye alikuwa mcheza muziki DJ fundi na alikabidhiwa vipindi vile vya ufundi wa kuchanganya muziki na mara nyingi wakati wa Weekend.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Radio lianza kukua kwa kasi huku Radio zingine zikianzishwa kukuza ushindani.Hivyo kituo kilihitaji darasa lingine kupambana na ushindani huo na darasa hilo lilikuja mwaka 1995 likinijumuisha mimi,Sunday Shomari na Peace Kwiyamba.Binafsi nilipewa jukumu la kusaidiana na Taji Liundi katika uchambuzi ndani ya vipindi mbali mbali,Sunday Simba Shomari alishirikiana na karibu kila kipindi kuleta mchangayiko na Peace alishirikiana kwa karibu na Deo "Best Friend" Mshigeni katika vipindi vya salamu na muziki wa taratibu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini mbali ya vipindi vya burudani uongozi wetu hapo baadaye uliona ni vyema baadhi yetu tukasoma taarifa za habari na kuripoti kupitia vipindi vya Current Affairs kama Nipashe n.k.Peace Kwiyamba na miye tulibahatika kuingia katika upande mwingine wa kituo na kuwa wasomaji kamili wa taarifa ya habari na maripota.Tulipata mafunzo yetu pale Radio Tanzania Dar Es Salaam chini ya wakufunzi kutoka chuo kikuu cha Whitwatersand kilichopo Afrika kusini.Mafunzo haya yalidhaminiwa na serikali kwa pamoja na mfuko wa Ebert Stiftung nchini Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Taji "Master T" Liundi alikuwa ni kivutio cha aina yake si tu kwa uwezo wake wa kuchambua mambo mbali mbali,bali pia kwa mahojiano yenye ukina na wanamuziki mbali mbali,uwezo wake wa kuongea lugha zaidi ya tatu na kwa ubunifu.Ikumbukwe yeye ndiye mwanzilishi wa neno "Chombeza",neno alilolibuni kumaanisha kubembelezana kiaina kati ya wapendanao hasa nyakati za usiku alipokuwa akipiga kipindi maalumu cha nyimbo za taratibu.Neno hili sasa ni maarufu sana huko Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Master T pia alikuwa na ushawishi mkubwa sana hasa kwa vijana ambao wengi walikuwa ni wasikilizaji wa vipindi alivyokuwa akiviendesha Radio One.Aliwalenga pia vijana waliokuwa na mwelekeo wa kuingia katika muziki wa kizazi kipya na hakusita kujitolea kuwashauri kwa ukaribu na hata kujichukulia muda wake wa ziada kushiriki kwenye mazoezi na wakati mwingine hata kuwalipia sehemu hizo za mazoezi.Kwa vile sasa tulikuwa timu moja Taji alinishirikisha sana katika mambo mbali mbali yahusuyo kazi na hata nje ya kazi.Tulikuwa bega kwa bega kwenye matamasha mbali mbali yaliyokuwa yakiandaliwa na vikundi vya utamaduni vya shule mbali mbali za sekondari jijini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ukaribu huu mkubwa kati yangu na Taji nia hasa ilikuwa ni kubadilisha mtazamo wa muziki Tanzania kwani mpaka wakati huo ni nyimbo za Marekani na nchi zingine za Afrika ndizo zilizokuwa zikichukua nafasi katika Radio One's Top Ten,Chaguo la msikilizaji na DJ Show vipindi ambavyo vilikuwa ni jahazi na vilibeba sura ya kituo.Vipindi hivi tuliviendesha kwa umahiri mkubwa huku tukipokezana na mwenzangu Master T.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabadiliko haya tuliyokuwa tukiyalenga ni yalikuwa hasa ni kujaribu kuupa nafasi muziki wetu hasa ule wa kizazi kipya katika show kubwa nilizozitaja hapo juu,lakini piajitihada zetu hazikuwa na mteremko hata kidogo bali vikwazo pia,vikwazo hivyo vilimweka Taji katika wakati mgumu zaidi na kufanya ajiulize mara mbili mbili kwamba yuko kwenye Radio yenye mabadiliko kwa manufaa ya nani zaidi kama si kizazi kipya?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nitatoa aina mbili ya vikwazo tulivyokumbana navyo kati ya vingi ambavyo havikutaka kutoa nafasi kwa wanamuziki wetu wa kizazi kipya kuutangaza muziki wao.Na vikwazo hivi zilifanya yeyote aliyetaka kwenda kinyume aidha kupoteza kazi,kusimamishwa kazi au kupewa onyo kali kwa maandishi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Mosi&lt;/span&gt;: Kutokana na mpangilio wa vipindi na kwa matakwa ya watayarishaji wakuu ilikuwa ni marufuku kupiga muziki wa ndani ya Tanzania zaidi ya ule wa dansi bila muziki huo kusikilizwa na mmoja kati ya watayarishaji na kuukubali.Zaidi ya hapo ni ruksa kupiga muziki wowote kutoka Afrika au Marekani mradi tu uwe ni clean version (toleo lisilo na lugha chafu).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;Pili&lt;/span&gt;: Si ruksa kufanya mahojiano na mwanamuziki wa kizazi kipya au asiyefahamika bila mwanamuziki huyo kufanyiwa usaili na watayarishaji (nikiwa na maana wakongwe) niliowataja hapo juu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hayo ni machache tu,lakini yalituweka katika wakati mgumu sana.Kitu kimoja tulikubaliana na watayarishaji ni suala la kutopiga muziki weneye matusi na sote tulilipinga hilo lakini kwa haya mengineyo hatukuwa katika level sawa.Wengi tulionelea kuwa pengine tunarudishwa enzi ya Radio Tanzania bila kujua na tulipanga kupigania hilo kwa nguvu zote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mimi na Taji tulipata barua kadhaa za onyo na hata kuhamishwa vipindi wakati fulani.Lakini hilo halikutuzuia kuongea kwa sauti juu ya kile tulichoona si haki.Tulitaka uhuru zaidi kwenye vipindi tulivyokuwa tukiendesha ili kipindi maarufu kama Top Ten yetu ipambwe na muziki wa kizazi kipya na mchanganyiko wa miziki ya aina zingine.Hiyo ilikuwa ni ndoto yetu kila kukicha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa jitihada hizi za kupigania muziki huu wa kizazi kipya uende hewani sambamba na aina zingine za muziki bila ukiritimba au masharti uituweka katika nafasi mbaya kiasi sio kazini tu bali hata mitaani ambako baadhi walituona kama tunaiga sana u-Marekani na kwamba kwa kutaka kupiga nyimbo kama hizi za kizazi kipya basi sisi ni wahuni tu na labda lengo letu kuu lilikuwa ni kutaka kuwafurahisha watu wa makundi yetu tu,kwa mtazamo wao watu wa makazi ya hali ya juu kama Oysterbay,Masaki n.k bila kujua binafsi nilikuwa nikiishi (Mbagala Kwa Makuka) mbali kabisa na maeneo wanayoyasema.Lakini lengo letu lilikuwa ni kutenda haki kwa kila mwanamuziki hata kama wa kizazi kipya bila kujali wasifu wa wanakotokea.Japokuwa mwanzo wao ulikuwa mgumu kwani mashairi katika nyimbo zao yalikuwa lege lege na kutokana na ufinyu wa viwango vya studio wakati huo midundo/mipigo ndani ya miziki yao ilionekana kutokuwa na mpangilio,lakini tulihoji kwa nini wasipewe nafasi tu kwanza halafu tuone jamii itawapokea vipi? ilikuwa si sahihi kukataa kuiga nyimbo zao na kufanaisha viwango vya urekodi na vile vya wanamuziki wengine wa kimataifa ambao nyimbo zao mpaka zilikuwa zikichosha.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mambo yalikuwa magumu na yasiyotabirika kutokana na harakati hizi.Hatimaye Master T aliondoka Radio One na kwenda jijini Mwanza ambako Radio (Radio Free Africa) nyingine ilikuwa ikianzishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya Master T kuondoka nilikabidhiwa vipindi vitatu mfululizo (DJ Show,Chaguo La Msikilizaji,na Top Ten) kuviendesha,kati ya hivyo DJ Show ilikuwa weekdays na vingine weekly,ilikuwa mshtuko na kwa kweli kazi ngumu lakini kwa vile nilipenda na bado naipenda sana kazi ya utangazaji sikusita kuendeleza kasi ile ile aliyoiacha Taji japokuwa siwezi kusema kuwa pengo lake lilizibika.Lakini tulikuwa bado tukibadilishana mawazo kila mara tukiongea kwenye simu akiwa Mwanza.Moja kati ya msisitizo katika kila mazungumzo yetu ilikuwa ni kukaza uzi na kamwe kutotetereka na yeye akianzisha mzimamo kama aliouacha huko Mwanza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mambo yalianza kubadilika na nadhani kwa sababu ya wakati pia.Makundi tuliyokuwa tukiyapigania ni makundi mawili makubwa na haya ni makundi ya mwanzo kabisa katika muziki wa kizazi kipya Tanzania ukiachilia mbali wale waliokuwa wakighani au kuimba bila kurekodi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kulikuwa na makundi ya Hip Hop kama Fresh XE Mtui,Kwanza Unit,Deplowmatz,Hard Blasters,Gangstar With Matatizo,Wagumu Weusi Asilia,Young Da' Mob,II Proud,Saleh Jabir,Samia X,Bugz Malone,Sos B,Afro Reign na flava kama za akina Mohd Momella,4Kruz Flava,Stara Thomas, Pamela na Mawingu Band,Connie Francis,Jungle Crewz Posse,Kamakazi Soldiers(6-7 years old kids),Mac Mooger,E-Attack,Afro Reign (chini ya Seba Maganga),Bantu Pound,Hardcore Unit/immeditation Kingdom nk.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia kulikuwa na makundi ya Reagge kama  Inno Nganyagwa,Pompidou,Kimbuteh &amp;amp; Roots Band,Justin Kalikawe,Innocent Galinoma (USA),Jontwa Jokeri,Makoya Man na wengineo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tusahahu kuwa hata muziki wa dansi uliingia katika kizazi kipya kwa kasi tofauti kabisa na kubadili mtazamo wa bendi kama Msondo na Sikinde.Nazungumzia band ya Diamond Sound,wana ikibinda Nkoi chini ya Eliston Angai.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati pengine hawa makazi yao yalikuwa Dar Es salaam ambako pia studio nyingi zilikuwepo,tukumbuke pia mikoani kulikuwa na ma-rapa waliokuja juu ile mbaya.Kwa vile nilisoma mkoani mbeya namkumbuka Rapa aliyekuwa akiitwa BBG ambaye alikuwa kibwagizo tosha kwenye ma-disco mjini Mbeya kama RTC,Mount Livingstone,AA Cool Para wa Zanzibar,Comtish wa ZNZ,pia kundi la Bombastic nk.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naweza kusema hawa ndio waliweza kufungua ukurasa mpya wa muziki wa kizazi kipya Tanzania na baadhi yao waliwahi kufanya mahojiano na Taji kabla hajaondoka kuelekea Mwanza na sio siri walikubalika japokuwa muziki wao ulianza kupigwa lakini sio sana kama ambavyo piganio letu lilitaka.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Japokuwa jitihada zilianza kuzaa matunda,kazi sasa ilikuwa kwa wanamuziki wenyewe kuhakikisha wanauweka ulimwengu wa Tanzania sawa na kwamba jitihada na harakati zetu za kuupigania muziki huu uende hewani haziangushwi na kushindwa kwao.Tuliwaasa kupiga muziki wa kueleweka wenye maadhi si ya ki-Marekani zaidi au nje zaidi bali muziki wenye mtazamo wa kitanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tulishauri kuwa ili muziki uwe na nafsi basi ni vyema tukaweka vionjo vya kwetu zaidi kama wenzetu wa Afrika ya Kusini na mtindo wao  Kwaito.Hata huko Marekani kulikuwa na mtindo tofauti kidogo wenye mahadhi ya hip hop ulioanzishwa na mkongwe  Teddy Riley unaoitwa "New Jack Swing" ambao ulibaki kam Hip Hop ila yenye vionjo tofauti na ladha ya New York.Nilitoa mifano hii makusudi kwenye kipindi maarufu nilichokuwa nikiendesha cha DJ Show kwa sababu walengwa na wadau wengi wa muziki Tanzania walikuwa wasikilizaji wakubwa wa kipindi hiki.DJ show ndio ilikuwa kilabu Raha Leo Show yao na nilisisitiza sana kwenye mapinduzi ya kuwa na mtindo wetu mpya wenye ladha yetu wenyewe.&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;br /&gt;&lt;/div&gt;&lt;div&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Inaendelea juu...&lt;/span&gt;&lt;/div&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-4283190478852580713?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/4283190478852580713/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=4283190478852580713' title='1 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4283190478852580713'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/4283190478852580713'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2008/06/ujio-wa-radio-za-masafa-mafupi-na.html' title='SEHEMU YA PILI.'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://bp1.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SFHhS3LP1DI/AAAAAAAAAAo/58rktFddAR8/s72-c/sc005a1d8a.jpg' height='72' width='72'/><thr:total>1</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-7197325948811424248</id><published>2008-06-10T17:07:00.000-07:00</published><updated>2008-07-03T19:17:58.881-07:00</updated><title type='text'>CHIMBUKO LA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA TANZANIA NA MAANA HALISI YA NENO BONGO FLAVA.</title><content type='html'>&lt;a onblur="try {parent.deselectBloggerImageGracefully();} catch(e) {}" href="http://bp3.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SE8k6b0ZObI/AAAAAAAAAAY/vedX6BV572U/s1600-h/026_27.JPG"&gt;&lt;img style="display:block; margin:0px auto 10px; text-align:center;cursor:pointer; cursor:hand;" src="http://bp3.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SE8k6b0ZObI/AAAAAAAAAAY/vedX6BV572U/s320/026_27.JPG" border="0" alt="" id="BLOGGER_PHOTO_ID_5210423880209480114" /&gt;&lt;/a&gt;&lt;br /&gt;(Pichani: Marehemu Cool James (James Dandu) akiwa nami baada ya kumtambulisha kwa mara ya kwanza nchini Tanzania ndani ya bwawa la kuogelea la Kilimanjaro Hotel.Dandu aliimba kwa mara ya kwanza kwenye onesho hilo.)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-weight: bold;"&gt;                                                                           SEHEMU YA I&lt;/span&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;   &lt;span style="font-weight:bold;"&gt;M&lt;/span&gt;oja kati ya mambo niyapendayo mno maishani ni muziki.Nimekuwa mfuatiliaji mzuri sana wa muziki si tu ule wa nje lakini kwa karibu ule wa nyumbani hasa muziki wa dansi na ule wenye umaarufu sana hivi sasa ujulikanao kama Bongo Flava (Muziki wa Kizazi Kipya).Katika mapenzi hayo imekuwa kama bahati kuwa mmoja wa vijana wengi tuliobahatika kuuona muziki huu wa kizazi kipya ukizaliwa na pengine bahati zaidi bila kusita kusema;kuwa mmoja kati ya wale tulioanzisha kusukuma gurudumu la muziki huu kufikia hapa ulipo na nafasi yake kutambulika si tu Afrika Mashariki bali pia kwa sasa duniani kwa ujumla.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama ilivyo kwa aina zingine za muziki Tanzania,mfano muziki wa dansi basi utakuwa mkosefu wa fadhila bila kujumuisha majina kama Patrick Balisidya,Mbaraka Mwaruka Mwinshehe,Salum Abdalah na hata Remmy Ongara.Hawa ni vinara na walifanya kila wawezalo kuja na ubunifu si tu kuvutia wateja wao bali kuutangaza muziki wao ndani na nje ya nchi na kuipa Tanzania kitambulisho chake kwenye jukwaa la sanaa ya muziki.Kazi za wanamuziki hawa zilifana sana kwa ushirikiano mkubwa na chombo ambacho kwa Tanzania ni muhimu sana katika kueneza au kutambulisha kitu kipya,RADIO.Watangazaji kama Mzee Ibrahim Chimgege,Enock Ngombale,Timothy Pata,Abisai Stephen,Seif Salum Nkamba na Julius Nyaisangah chini ya ma-bwana mitambo mahiri kama akina James Mhilu na Crispin Lugongo wanastahili pongezi kwa kiasi kikubwa katika kurekodi na kusimamia mitambo wakati wanamuziki hawa wakitafuta majina na namna ya kujitambulisha kwa jamii itakayosikiliza muziki wao.Bahati mbaya huwasikii sana watu hawa katika zinazoitwa historia kwa sababu wengi ni rahisi kuwasahau lakini mchango wao ni mkubwa sana na unastahili heshima hasa unapoandika au kuizungumzia historia ya muziki wa dansi Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nimetoa mfano wa hali halisi kwa ufupi kuhusu muziki wa dansi ili kukupa nafasi ya kujua kwa undani kile ambacho kinakweza kichwa cha habari hapo juu.Nia yangu hasa ni kuandika yale niliyoyaona na uzoefu wangu katika muziki huu wa sasa maarufu kama Bongo Flava.Muziki huu umeshika kasi na unapendwa sana hivi sasa kila kona.Ni faraja kuona hata wale walio ughaibuni siku hizi si ajabu kumkuta mtu ana albamu jpya la mwanamuziki wa Bongo Flava akiicheza ndani ya nyumba yake au garini kwa fahari.Inafurahisha kuona mapenzi kwa muziki huu yamekuwa makubwa na hilo ndilo lengo kuu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na yote haya,kama ilivyo kwa kila jambo ni vyema historia yake ikawa nyoofu na si kama ilivyo sasa ambavyo imekuwa ikipindishwa pindishwa mno,sijui kama ni kwa makusudi au kwa wengi kutojua harakati na wanaharakati walioufikisha muziki huu hapa ulipo.Kwa kuandika kwa usahihi yale yaliojiri juu ya chimbuko la muziki huu tutakuwa tunawatunzia wanetu na wengineo haki ya kuuelewa na kuutukuza zaidi muziki huu na msimamo wake katika jamii ya leo na ijayo.Shukrani labda nizitoe kwa Kaka Bonny Makene na Uncle michuzi kwa kunisukuma kujaribu kuandika nikijuacho juu ya muziki huu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kama nilivyododosa hapo juu kuhusu muziki wa dansi basi sasa niingie kwenye muziki huu wa kizazi kipya.Muziki huu ni ule ambao unajumuisha mitindo mbali mbali ambayo zamani tulizoea kuona ikipigwa na watu wa nje ya Tanzania kuanzia Hip Hop,R&amp;amp;B,Zouk na hata Soul.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika Hip Hop ya Tanzania pia utakosa fadhila kama hutotaja vijana wa mwanzo kabisa ambao kuanzia mivao yao na kufoka foka kwao kulikuwa ni burudani na ushawishi tosha kwa watu kuanza kudadisi kuhusu maana halisi ya utamaduni huu hasa Tanzania.Kwa wakati huo ilionekana kama uhuni tena wa kupita kiasi.Nitawataja wachache ninaowakumbuka ambao kila kukicha ukigongana nao kwenye Night Clubs,Samora Avenue pale Salamander basi ulikuwa unachoka mwenyewe.Nakumbuka vijana kama John Simple,Dj Rusual,The BIG One,Babu Manju,David Nhigula,Abdulhakim Magomelo,Kessy,Ibony Moalim,Tom London,OPP (now Jay P) na Dj Ngomeley.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tukiendelea hao niliowataja hapo juu walikuwa chachu katika uvaaji wa kihip-hop na katika kughani na sijui kama kuna mtu atasahau watu kama Fresh XE Mtui,BBG (alianza na Mr II),Adili kumbuka,KBC (Mbeya Tech),Saleh Jabir,Samia X,THE BIG,Rhymson,2Proud.Deplowmatz na wengineo wengi ambao walikuwepo na wakighani katka school parties au matamasha ya mtaani kabla hata ya kurekodi nyimbo zao studio.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa mara ya kwanza pia promoters kama Joe Kusaga na Abdul hakim Magomelo walionekana kutobaki nyuma katika ukuzaji wa sanaa hii ambapo waliandaa matamasha mbali kama Yo! Rap Bonanza na Coco beach Bottle Parties kwa ajili ya kuwapa nafasi wale wenye uwezo wa kughani.Matokeo yake yalikuwa ya kufurahisha kwani kila mmoja alikuwa na shauku ya kuingia katika gemu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa vile sio watu wote walikuwa na uwezo wa kughani lakini pia kulikuwa na wale wenye kuimba kama wanamuziki wengi wa Marekani kwa kupitia matamasha mbali mbali kwenye Jumba la utamaduni la Urusi,Korea na mengineyo yalikuwa yakiandaliwa hasa na wanafunzi wa shule mbali mbali za sekondari jijini kama Forodhani pia matamasha yaliyokuwa yakifanyika kando kando ya ufukwe ambako wengi wenye kutaka kuimba walijitokeza.Hapa tunakumbuka kundi kama la Mawingu na mwana dada Pamela,mwanadada Stara Thomas na Judith Wambura ambao uwezo wake wa kughani na kuimba kama Mc Lyte ulimpa tafu hasa alipofanya hivyo kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha DJ show ya Radio One,shukrani kwa Ipyana Malecela Mkwavi (RIP) kwa zawadi ya LP yenye instrumental (ala) tupu aliyonipatia kama zawadi aliporudi toka UK kwani instrumental ya single "Keep,Keeping on" ndiyo iliyomtambusliha Jay Dee wa leo Radioni kwa mara ya kwanza japokuwa kabla ya hapo alikuwa mwimbaji wa kwaya kanisani lakini mweye kusita kuingia kwenye muziki wa kidunia.Pia Kundi la R&amp;amp;B lililojulikana kama Four Krewz Flava pia Herbert Makange ambaye pia alikuwa akiimba.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naweza nikawa nimesahahu majina machache hapo juu lakini kwa ufupi hao ni baadhi ya watu wa mwanzo kabisa kuuingiza masikioni mwa jamii muziki wa kizazi kipya pengine hata kabla ya chombo kilichoipaisha juu zaidi..RADIO.Na ninaposema Radio simaanishi Radio nyengine bali Radio One Stereo kama Radio pekee yenye kujivunia juu ya ukuaji wa muziki huu wa kizazi kipya kufikia hapa ulipo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini uko nako hakukuwa na mteremko,mambo yalikuwa mengi na mazito mpaka muziki kujipenyeza na kukubalika.Je nini kilichochea mapambano ya kuuchomeka muziki huu Radioni na kuupa nafasi ya kupigwa sambamba aina zingine za muziki kama ule wa dansi nk?  nani alihusika katika harakati hizo na nini kilifuata? ugumu huo ulitokana na nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;span class="Apple-style-span" style="font-style: italic;"&gt;Inaendelea juu.....&lt;/span&gt;&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-7197325948811424248?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/7197325948811424248/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=7197325948811424248' title='0 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/7197325948811424248'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/7197325948811424248'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2008/06/chimbuko-la-muziki-wa-kizazi-kipya.html' title='CHIMBUKO LA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA TANZANIA NA MAANA HALISI YA NENO BONGO FLAVA.'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><media:thumbnail xmlns:media='http://search.yahoo.com/mrss/' url='http://bp3.blogger.com/_unbAPpKBNZ4/SE8k6b0ZObI/AAAAAAAAAAY/vedX6BV572U/s72-c/026_27.JPG' height='72' width='72'/><thr:total>0</thr:total></entry><entry><id>tag:blogger.com,1999:blog-6656507346177831709.post-6415286955451016721</id><published>2008-06-05T18:07:00.000-07:00</published><updated>2008-07-04T17:38:42.204-07:00</updated><title type='text'>Hodi Hodi Ukumbini.</title><content type='html'>Habari wana-blog.Najaribu tu kuingia mtandaoni kwa ushawishi wa wakongwe katika hii fani (Uncle Michuzi,Makene,Babu,KBC,Kaka Jeff Msangi na wengineo).Nia kubwa ni kubadilishana mawazo na waungwana katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia juu ya mambo mbali mbali yanayotuzunguka katika maisha yetu ya kila siku kuanzia muziki mpaka siasa.Shukurani kwa nyote mlionishawishi nami nijiunge kwenye jumuiya ya ku-blog.Karibuni ndani ya ....Yangu Macho!&lt;div class="blogger-post-footer"&gt;&lt;img width='1' height='1' src='https://blogger.googleusercontent.com/tracker/6656507346177831709-6415286955451016721?l=pesambili.blogspot.com' alt='' /&gt;&lt;/div&gt;</content><link rel='replies' type='application/atom+xml' href='http://pesambili.blogspot.com/feeds/6415286955451016721/comments/default' title='Post Comments'/><link rel='replies' type='text/html' href='http://www.blogger.com/comment.g?blogID=6656507346177831709&amp;postID=6415286955451016721' title='3 Comments'/><link rel='edit' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/6415286955451016721'/><link rel='self' type='application/atom+xml' href='http://www.blogger.com/feeds/6656507346177831709/posts/default/6415286955451016721'/><link rel='alternate' type='text/html' href='http://pesambili.blogspot.com/2008/06/hodi-hodi-ukumbini.html' title='Hodi Hodi Ukumbini.'/><author><name>Karibu</name><uri>http://www.blogger.com/profile/10649000543167255034</uri><email>noreply@blogger.com</email><gd:image rel='http://schemas.google.com/g/2005#thumbnail' width='16' height='16' src='http://img2.blogblog.com/img/b16-rounded.gif'/></author><thr:total>3</thr:total></entry></feed>
